Pages

Thursday, May 9, 2019

AISIIIII……….U KILL ME 18........ ONLY 18+

ILIPOISHIA
Kabla sijamjibu mama kitu chochote macho yangu, yakawa yanamuangalia muhudumu wa kiume anaye kuja eneo nililo kaa na mama, huku mama akiwa amempa mgongo muhudumu huyo aliye beba sahani pana huku juu yake ina chupa ya whyne pamoja na glasi mbili na chini ya sahani hiyo kuna kitaulo kidogo cha kufutia mezani, ila ndani ya kitaulo kwa umakini sana nikaona bastola, iliyo fungwa kiwambo cha kuzuia risasi, kikiwa kimefungwa. Pasipo kusubiria aweze kutekeleza lengo ambalo linamleta mezani kwetu nikachomoa bastola yangu kiunoni na kumpiga risasi mbili za miguuni na kumfanya anguke, huku chupa, sahani, glasi na bastola yake vikiangukia pembeni. Ila mlio wa risasi bastola yangu ambayo sijaifunga kiwambo cha kuzuia sauti, ukawafanya watu walio kuwepo katika eneo hilo kutawanyika kwa woga, huku mama akiwa ameshikwa na bumbuazi akinitolea macho.

ENDELEA
Nikanyanyuka kwa haraka kwenye kiti nilicho kalia huku nikitembea kwa tahadhari bastola yangu ikiwa mikononi nikimsogelea muhudumu huyo. Nikachuchumaa, na kumgeuza kwa maana amelala kifudifudi. Nikamkuta muhudumu huyo akiung’ata ulimi wake kwa ajili ya kujiua. Nikajaribu kumzuia kujiua ila nikawa nimesha chelewa kwa maana tayari alisha ng’ata kipande cha ulimi wake na kukimeza na kusababisha damu nyingi kumwagika umdonini mwake.
Nikakumbuka maneno ya mwalimu wangu kipindi nipo chuoni nina somea maswala ya upelelezi, aliniwahi kuniabia kwamba maadui wapo wa aina nyingi, ila endapo maadui hao wanapo jikuta wanakaribia kuingia mikononi mwa askari, mbinu yao ya kwanza kuifanya ni kuung’ata ulimi na kuumeza, kitu kinacho peleka wao kufa haraka pasipo kuzungumza kitu cha aina yoyote ili kuto kutoboa siri.
Nilipo ona hivyo nikaachana naye na macho yangu yakawa na kazi ya kutazama maeneo mbali mbali ya hoteli hiyo ili kuweza kuona kama kuna maadui wengine wapo katika eneo hilo. Nikarudi sehemu alipo mama, na kumshika mkono na kumnyanyua kwenye kiti alicho kali.
“Mama tuondoke hii sehemu sio salama”
“Dany ni nini umefanya?”
“Mama tuondoke”
Nilimshika mama mkono na kuanza kutoka naye katika eneo hili, huku bastola yangu ikiendelea kuwa mkononi na muda wote nikiwa makini sana kwa kumtazama kila mtu aliyopo mbele yangu na muda mwengine nikalazimika kugeuka nyuma na kuangali kama kuma mtu ambaye anaweza kufanya shambulizi. Nikiwa hapo nikakutana na askri waona linda hoteli hii, wote ambao ni wanne wakaninyooshea bunduki zao na kuniomba nisimame na niweke bastola yangu na mikono yangu niiweke juu.
Kutokana ni moja wapo ya sheria, pale unapo kunata na kitengo kingine cha ulinzi ambacho hawakufahamu wewe ni nani, ikanilazimu kuweka bastola yangu chini na kuinyoosha mikono yangu juu kwa haraka huku mama yangu akiwa amesimama pemebeni.
“Jamani huyu ni askari”
Mama alizungumza kwa kunitetea, kutokana ni mkuu na anajulikana hata kwa askari hao, kidogo wakaanza kuniamini ila bado mitutu ya bunduki zao wakiwa wamenielekezea.
“Muheshimiwa hujaumia?”
“Sijaumia huyu ni kijana wangu”
Kwa haraka ikanibidi kutoa kitambulisho changu ambacho popote ninapo kwenda huwa ninakibeba, kwa ajili ya kujilinda pale nitakapo kamatwa. Askari hao walipo ona kitambulisho changu wakaniamini na kuniomba msamaha. Nikaokota bastola yangu, kisha nikasimama huku ninawatazama kwa macho makali yaliyo waogopesha hata askari hao ambao ni wakampuni ya ulinzi hapa Tanga. Tukiwa hapo tukasikia kelele kwenye moja ya chumba na akatoka msichana mmoja ambaye ni muhudumu huku anakimbia. Nikamuwahi kwa kumdaka na kumziba mdomo asipige kelele.
“Kuna nini?”
“Luka kafaaa, wamemuua Luka”
Msichana huyo alizungumza huku akilia, ikatubidi mimi na askari hao kwenda katika chumba hicho ambacho anadai ndipo alipo uwawa huyo Luka. Tulipo ingia, tukakuta mauaji ya kikatili sana kwa maana kichwa cha mfanyakazi huyo kimekatwa na kuwekwa juu ya meza huku kiwili wili chake kikiwa kmelazwa sakafuni na akiwa amevuliwa nguo zote na kubakiwa na boksa.
“Huyu ni nani?”
“Ni muhudumu wa hii hoteli”
Hapo ndipo nikapata picha kwamba yule muhudumu niliye mpiga risasi, si muhudumu wa hoteli hii bali alimuua huyu Luka kisha nguo za muhudumu akavaa yeye. Kwa haraka nikaanza kukagua chumba hicho kuweza kupata japo kijiushahidi, kwa bahati nzuri nikapata waleti iliyo angushwa na ipo chini ya kitanda. Nikaifungua na kukutana na passport y ya kusafiria ya jambazi niliye muua, nikakuta ni raisi wa Somalia na ameingia nchini Tanzania siku tano zilizo pita, nikakuta vikaratasi vingine vingine vikiwa vimeandikwa lugha ya kiarabu.
“Pigeni simu polisi”
“Tayari imesha pigwa”
Nikatoka katika chumba hicho na kurudi mapokezi ambapo nikamkuta mama akiwa amekaa kwenye moja ya kiti ametulia akionekana ana mawazo mengi sana.
“Mama tuondoke”
“Kuna nini huko chumbani?”
“Kuna muhudumu mmoja ameuwawa na yule jamaa niliye mpiga risasi”
“Mungu wangu, sasa kwa nini wamefanya hivi?”
“Hao wapo kwa ajili yako wewe”
Mama akanishangaa huku akiwa kama haamini kitu ambacho ninakizungumza ila huo ndio ukweli halisi ambao tayari nimesha ugundua. Tukaingia kwenye gari na kuondoka eneo hilo, tukiwa njia tukapishana na gari za polisi mbili zinazo elekea eneo la hoteli hiyo zikiwa katika mwendo wa kasi.
“Mama hapa inabidi nikupeleke kwa baba mkubwa Eddy ukakae huko kwa muda”
“Sawa”
Mama alijibu kiunyonge tayari woga ulisha mjaa. Nikazidi kuongeza mwendo kasi wa gari huku muda wote nikiwa makini sana katika hilo. Tukafika nyumbani kwa baba mkubwa ambapo ni maeneo ya Nguvumali karibu na ikulu. Nikapiga honi ambapo mlinzi akafungua geti na tukaingia, gari nikalisimamisha maeneo ya maegesho ya magari. Nikashuka na mama naye akashuka kwa bahati nzuri tuliweza kumkuta baba mkubwa akiwa amekaa kwenye moja ya bustani yake akijisomea vitabu. Tukatembea hadi eneo alilopo, alipo niona akatabasamu kwa maana ni muda mrefu sana hatujaonana.
“Shikamoo baba”
“Marahaba, Dany siku hizi huji kabisa nyumbani kwangu”
“Shemeji shikamoo”
“Marahaba shemeji, karibuni”
“Asante”
“Baba mkubwa si unajua mizunguko yetu hii ya kibiashara kidogo inatuweka bize sana”
Nilizungumza hivyo kutokana mtu pekee anaye ifahamu kazi yangu ni mama yangu mzazi tu, hadi mdogo wangu wa kike alifahamu hilo.
“Ahaa uwe unakuja hata kututembelea, au unataka kusikia kwamba baba yako mkubwa nimekufa ndio uje?”
“Hapana baba leo nimeamua kuja na mama, tutalala huku”
“Ahaa, Shemeji ni kweli anayo yazungumza mtoto hapa?”
“Ni kweli shemeji, alikuja juzi leo basi analalamika anataka kuja kulala huku”
“Karibuni sana, tena mama yako mkubwa naye ametoka Marekani jana yupo huko ndani na wanae”
“Ahaa basi ngoja nikawaone”
Nikanyanyuka na kumuacha mama na baba mkubwa, nikaingia ndani bila hata kubisha hodi nikamkuta mama mkubwa na mabinti zake wawili mapacha ambao nimewapita umri wakipiga stori sebleni, walipo niona kwa haraka wakanyanyuka na kunikimbilia huku wakiwa na furaha.
“Kaka Danyyyy”
Xaviena na Xaviela ambao ni watoto wa baba mkubwa Eddy, wakanikumbatia huku wakiwa na furaha sana kwa maana ni kipindi kirefu sijaonana nao.
“Jamani kaka Dany umetususa, hupigi simu wala kuwasiliana na sisi?”
“Xaviena si unajua maisha mdogo wangu, maisha ni magumu”
Nilizungumza huku wakiwa wamenishika mkono na kueleka nao kwenye masofa yaliyopo hapo sebleni. Nikamsalimia mama mkubwa ambaye anaitwa Rahma.
“Marahab, Dany umekua haraka haraka?”
“Msosi mama”
“Hata mimi naona, vipi umekuja na mama?”
“Ndio nimekuja naye wapo hapo nje na baba mkubwa”
“Wacha nikamsalimie, tena nilikuja na zawadi yake kutoka Marekani”
“Ya kwangu ipo wapi?”
“Mmmm wewe umesaulika na kukaa kwako kimya”
Mama mkubwa akatoka na kuniacha nikiwa nimekaa na wanae hawa mapacha wanao fanana sana na kama mtu hujawazoea basi utawachanganya sana. Nikaona picha ya Xaviena akiwa amevalia taji la umesi ikiwa imebandikwa ukutani.
“Xaviena umesha wahi kuwa miss kumbe?”
“Ahaaa tena sasa hivi tupo kwenye mikakati ya kugombania umiss Tanzania”
“Wacha weee”
“Ndio”
“Xaviela na wewe?”
“Mimi nipo nipo tu”
“Dany sasa hivi una misuli, kipindi kile ulikuwa kimbau mbau”
“Hahaaa napiga tizi gym sasa hivi”
“Nichukue basi na mimi nikapige tizi Gym”
“Xaviela unataka kupiga gmy?”
“Yaa mbona nimesha anza”
“Waoo basi, nipo Tanga tutawasiliana”
“Tupatie basi namba yako ya simu”
Nikatoa simu yangu na kuanza kuwatajia kila mmoja akaingiza namba yangu kwenye simu yake na kila mtu akanipatia simu yake. Kabla sijaingiza simu yangu mfukoni, ikaanza kuita na anaye piga ni K2, nikanyanyuka na kueleka chooni kuzungumza naye.
“Baby mbona kimya jamani?”
“Honey si unajua nyumbani huku, nipo na mama yako mkwe basi nakosa hata muda wa kupiga simu”
“Wee upo na mama mkwe alafu unaongea na simu mbele yake?”
“Hapana kwa sasa nimesogea pembeni kidogo”
“Ahaa, nimepata taarifa muda huu, nasikia tanga kuna mauaji yametokea kwenye hoteli moja waiita…….”
“Wanaiitaje?”
“Ahaa nimesahau jina nikikumbuka nitakuambia. Ila kuwa makini mpenzi wangu, hapa nilipo yaani nina kukumbuka, natamani hata uje”
“Usijali nitakuja siku si nyingi”
“Ila vipi kidonda?”
“Nimechomwa sindano za kutosha”
“Pole mwanya ehee”
“Asante honey”
“Poa honey baadae”
“Sawa baby I love you”
“I love you too honey”
Nikaka simu, kitendo cha kufungua mlango nikakutana na Xaviela na Xaviena mlangoni wakiwa wamesimma, kumbe muda wote walikuwa wananisikiliza.
“Dany unamchumbaaaa”
Xaviela alizungumza kwa kunitania huku akitabasamu. Wote wakaanza kucheka na kunifanya nicheke.
“Sasa ulikuwa unakimbia nini, si ungezungumza mbele yetu tumjue wifi yetu ni nani?”
“Acheni hizo bwana”
“Tunamuambia baba”
“Weee Xaviena musimumbie mzee bwana, mbona unataka kumwaga mchele mbele ya kuku wengi”
“Kama ni hivyo mpigie tena mchumba wako tuzungumze naye”
“Ahaa mbona munataka kunizinguza wadogo zangu”
“Kubaliana na sisi mpigie, au tumueleze mama mdogo na baba kwamba Dany una mchumba”
Nikashusha pumzi haraka hara huku nikiwatazama, kusema kweli nina wafahamu Xaviela na Xaviena, huwa wakilikazania jambo huwa hawapendi kuliachia, lipite kirahisi. Nikakumbuka nina namba ya Mariam, kwa haraka nikaitafuta na kumpigia, kwa bahati nzuri simu ya Mariam ikaanza kuita. Sikutaka wazungumze na K2 kwa maana kwanza sauti yake dhairi inaonyesha ni mtu mzima pili ana wivu sana na mimi kuliko hata mume wake wa ndoa. Maria akapokea simu kitu cha kwanza aliuliza mimi ni nani.
“Dany”
“Ohoo jamani honey za safari?”
Macho ya Xaviela na Xaviena yakawa yananitazama kwa umakini kwa maana wanahisi kama nina watania, ilinibidi kulipotezea swali la Mariam.
“Wifi zako hapa wanataa kukusalimia”
“Waoo wifi zangu, wape simu”
“Poa, nani aanze kuzungumza”
“Mkubwa kwanza”
Xaviela alizungumza huku akiichukua simu yangu na kuanza kuzungumza na Mariam, alimuhoji maswali mawili matatu kisha akamuachia Xaviena, ambaye naye maswali aliyo uliza mwenzake ndio aliyo uliza yeye, kisha akanirudishia simu.
“Dany mbona wifi zangu sauti ni kama mtu mmoja?”
“Mapacha hawa”
“Weeee, ndio maana sauti zao zinafanana”
“Ndio, sasa ngoja nitakupigia baadae”
“Sawa honey”
Nikakata simu na kuwatazama Xaviela na Xaviena
“Mume ridhika sasa?”
“Sanaaa”
“Twendeni nje, kuna sehemu nataka kwenda mara moja”
“Unataka kuondoka hivyo?”
“Hapana leo nalala huku”
“Kweli?”
“Ndio”
Nikatoka nao nje, tukaelekea kwenye bustani walipo kaa wazazi huku nikiwa nimewashika mikono. Tulipo fika wakamkumbatia mama kisha wakaka kwenye vitu vya pembeni. Nikawaaga na kuwaeleza kuna wafanya biashara ninakwenda kuonana nao, wote wakakubaliana name, ila mama pekee ndio anajua ni kazi gani iliyopo mbele yangu ambayo ni kuhakikisha ninazipata nyaraka zote zilizo ibiwa chumbani kwake.
Nikaingia kwenye gari la mama na kuondoka, safari hii nikielekea moja kwa moja katika mtaa wa nyumbani kwetu nikaliacha gari la mama kwenye moja ya baa inayo itwa Mwika, kisha nikaanza kutembea kwa miguu hadi eneo la karibu kabisa la nyumbani kwetu. Kigiza tayari kilisha anza kutawala angani nikaka kwenye moja ya nyumba iliyopo karibu na nyumba yetu, lengo langu ni kutaka kujua kama Yudia yupo au laa. Haukupita muda sana taa za nyumbani za nje ya nyumba zikawashwa, nikatambua kwamba yupo, ila nikiwa hapo nikaona gari nyeusi ikisimama nje ya geti. Akashuka jamaa mrefu kiasi na kuingia ndani humo na gari hiyo ikaondoka. Gari ilipo potea mbele ya macho yangu nikaanza kutembea kwa mwendo wa kasi hadi getini, nikachungulia kwenye kijiuwazi kidogo cha getini nikamuona jamaa huyo akizungumza na Yudia, ambaye anaonekana kufahamiana na mtu huyo.
“Ni upumbavu mulio fanya, munge muua. Sasa hii ni nafasi ya mwisho jifiche kwenye hiyo bustani wanarudi muda si mrefu. Sasa ole wako ufanye makosa nitakuua”
Maneno ya Yudia yalinifanya niishiwe nguvu kabisa kwa maana yale mawazo mabaya niliyo kuwa nina muwazia kumbe ni kweli na yeye ndio anahusika na mpango wa mauaji ya mama, nikatamani kuingia ila nilihisi kushindwa kabisa kwa maana jamaa huyo amejificha katika uwa kubwa lililopo kwenye bustani iliyopo karibu na getini na yoyote atakaye ingia ndani hapo ni rahisi kumuona ila mtu anaye ingia si rahisi kuweza kumuona muuaji huyo.
ITAENDELEA

No comments:
Write comments

Recommended Posts × +