Pages

Thursday, May 23, 2019

AISIIIII……….U KILL ME 30........ ONLY 18+

ILIPOISHIA
Wakati huu tunatembea kwa spidi themanini, hatufanyi upuuzi wa kumkimbiza raisi wa nchi kwa mana akipata taizo basi serikali ya jamuhuri itatuhukumu sisi. Tukiwa maeneo ya kukaribia kufika Nguvumali, yukaona gari mbili zilizo jaa wapiganaji wa kisomali zikija mbele yetu, jambo lililo anza kumpa wasiwasi kila mmoja na kama ninavyo fahamu kuna mpango mbaya umepangwa kwa ajili ya kumuangamiza raisi.
“Dany tanua barabara”
“Sawa”
Nikafanya kama alivyo niambia Babyanka, gari zetu zote zikatawala barabara huku kila mmoja akiwa makini kuhakikisha kwamba tunamuokoa raisi pili hawa wajinga wote safari yao ya kuingia Tanzania kinyemera inaishia hapa.

ENDELEA
Uzuri wa agri zetu tunazi zitumia, haziingii risasi hata kwenye vioo. Hichi ndio kitu cha kwanza kinacho tupa jeuri ya kufanya hiki tunacho kifanya kwa sana. Mwanga mkali wa gari zetu ukawafanya madereva wa gari hizi za Wasomali kujaribu kutukwepa, jambo lililo tupa nafasi mimi na Babyanka kila mmoja kuweza kudili na gari moja. Kwa kasiya ajabu niklipeleka gari langu kule kule anapo elekea dereva huyu na kumfanya ashindwe kulihimili gari na kujikuta akiparamia mti na kuanguka. Wapiganaji wa kisomali ambao walikuwa wakiruka ruka kutoka kwenye hilo gari kuyaokoa maisha yao, kila mmoja aliweza kupata majeraha yake kivyake. Nikafunga breki za gari pasipo kuuliza mimi na mlinzi mwenzangu wa raisi tukashuka kwenye gari huku tukiwa na bastola zetu mikononi. Hatukuwa na jambo la kufanya zaidi ya kuhakikisha kwamba tunawateketeza wapiganaji wote wa Al-Shabab. Kazi haikuwa ngumu kwa maana wengi walichanganyikiwa hawakutarajia kama kutatokea shambulizi la namna hii. Nikatupia macho upande upande wa pili wa kina Babyanka nikaona nao kazi yao wakiwa wanaimalizia malizia.
Tukaanza kukagua maiti moja baada ya nyingi, raisi akashuka kwenye gari huku akiwa haamni kazi ambayo tumeifanya vijana wake. Tupo wanne ila tumeweza kususha watu zidi ya thelethini.
“Muheshimiwa hii ndio hali ya nchi yako”
Nilimuambia raisi huku nikimuonyeshea maiti zilizo zagaa chini wengine wakiwa bado ni vijana wadogo wa mika kama kumi na mbili hivi.
“Haya yote unataka kunieleza kwamba yamefanywa na viongozi wangu?”
“Ndio muheshimiwa”
Nikamuona raisi jinsi sura yake ikibadilika kwa hasira, hakuzungumza kitu chochote zaidi ya kurudi kwenye gari. Akatuamrisha kuondoka eneo hili kabla hatujaonekena, tukatii amri na safari ikaendelea. Mara kadhaa nikawa na kazi ya kumtazama raisi kupitia kioo cha juu kidogo mbele yangu, ambacho kinaniwezesha kuona siti za nyuma.
Tukafika nyumbani kwa baba mkubwa, raisi akawasiliana na baba mkubwa na kumfahamisha kwamba aamesha fika. Ndani ya a dakika tatu geti likafunguliwa, taratibu tukaziingiza gari zetu kwenye jumba hili la kifahari ambapo sasa nikakuta ulinzi umezidi kuimarishwa.
Nikamuona baba mkubwa akiwa na mama mkubwa wakija katika gari zetu zilipo simama, sikutamani kushuka ila sikuwa na jinsi kwa maana kazi yangu ni kumlinda raisi na si kuionea haya familia baba mkubwa. Nikawa mtu wa kwanza kushuka kwenye magari, moja kwa moja nikazunguka upande wa mlango wa raisi na kumfungulia raisi mlango. Baba mkubwa na mama mkubwa wakabaki wakinishangaa, walihisi labda wamenifananisha, ila nikazidi kujikausha kama siwafahamu vile. Wakapeana mikono na raisi, wakamkaribisha wakiwa na furaha. Walinzi wote wanne muda wetu wote tukawa tunatazama kila kona ya eneo la hili jumba. Tukakaribishwa ndani, mimi na Babyanka tukaingia na raisi sebleni huku walinzi alio kuja nao raisi wakibaki nje wakiwa wamesimama mlangoni.
Nikamkuta mama, Xaviela na Xaviena wakiwa wamekaa kwenye masofa naamini waliutambua ujio wa rasii. Walipo niona wote watatu wakastuka, ila mama hakustuka sana kwa maana ananitambua vizuri. Kama wanavyo nifananisha baba mkubwa na mama mkubwa basi ndivyo Xaviela na Xaviena wanavyo nifananisha, wakatamani sana kuweza kuniita ila` wakashindwa kutokana na uwepo wa raisi.
“Karibu bwana muheshimiwa”
“Nashukuru sana, mabinti wako wamekuaa asiee, si ndio wale waliokuwa wadogo miaka ile”
“Ndio muheeshimiwa”
“Kweli watoto wasikuhizi wanakua haraka sana”
“Mkurugenzi habari?”
“Salama tu muheshimiwa karibu sana Tanga”
“Asante, nasikia ulipata misukosuko juu ya nyaraka za bandari?”
“Ni kweli muheshimiwa”
“Haina tabu kabisa hapo, nimekuja kutumbua majipu rasimi Tanga”
“Tutafurahi muheshimwia kwa maana sisi watendaji tulio chini ya mkuu wetu wa mkoa basi tunapata tabu sana”
“Huyo ndio jipu la kwanza, na nitalisweka gerezani, nilipo seme hapa Kazi tu, nilikuwa ninamaanisha hapa kazi, wala sibabaishi”
“Ni kweli muheshimiwa tunashukuru”
“Utendaji wako mimi bwana naufahamu toka siku nyingi, sasa ndugu yangu alikosea kukupa huu ukurugenzi wa jiji, nitahakikisha ninakupa mkoaa huu uunyooshee. Kwa maana nimeona kuna mambo mengi ya ajabu ajabu, ndio maana nimekuja usiku huu”
“Kweli muheshimiwa”
“Mama unaweza kutupisha na mabinti zako tukazungumza mambo kidogo ya kiserikali?”
“Hakuna shida muheshimiwa”
Mama mkubwa na wanae wakanyanyuka na kupandisha gorofani, tukabaki watu watano sebleni, huku mimi na Babyanka tukiwa kimya tunaangalia ulinzi wa ndani hapa.
“Nitakapo kupa uongozi wa mkoa, hakikisha bandari inaisha na ianaanza kufanya kazi mara moja. Imarisha ulinzi maeneo ya bandarini hapo, na pembeni pembeni ya bahari kwani kuna kundi la Al-Shabab vijana wangu wamewadhibiti hapo juu juu”
“Al-shabab mueheshimiwa!!?”
Mama aliuliza kwa kushangaa kwa mana naamni hafahamu ni kitu gani kinacho endelea katika mkoa wake nahisi alihisi misukuko suko ya mkuu wa mkono na Meya ambaye kwa sasa yupo ahera, ni ya kawaida tu.
“Ndio, kijana wangu hawa wawili ndio watakao nilinda katika dhiara nzima, na saa kumi na moja naamkia Bombo hospitali hapo kutumbua majipu”
“Sawa sawa mkuu tutakuwa pamoja”
“Ila kuna huyu mkuu wa polisi naye vipi?”
“Huyo atawajibika kijeshi, naye nitamtumbua”
Baada ya hapo mazungumzo yakaendelea ya kawaida huku wakipiga stori, hapakuwa na tu aliye weza hata kusinzia.
“Muheshimiwa hivi unajua huyo hapo ni kijana wangu wa kumzaa”
“Weee kweli?”
“Ndio muheshimiwa”
“Shemeji unataka kuniambia kwamba Dany ni afisa mzuri tena anaye mlinda raisi?”
“Ndio mwenyewe si huyo hapo muulize”
Nilibaki kutabasamu huku nikimtazama baba mkubwa kwa maana hakuamini kabisa kama nina uwezo wa kumlinda raisi.
“Hapa una jina asiee kwa mana amepambana kuwaangamiza hao Al-Shabab, naamini polisi watakuwa huko wakitazama maiti zao”
Raisi aliendelea kunimwagia sifa. Ikatimu saa kumi na moja kasoro raisi akaamrisha msafara wa kuelekea hospitali ya Bombo kuanza. Mama na baba mkubwa nao wakaingia kwenye gari lao, na kuongozana na nasi kuelekea hospitalini huko. Safari hii ikatubidi kubadilisha njia na kupita njia nyingine. Hadi inatimu saa kumi na moja na dakika tano tukawa tumesha fika katika hospitali ya Bombo. Nikashuka kwenye gari na kumfwata mlinzi, nikamuonyesha kitambulisho changu.
“Saa hizi sio muda wa kuona wagonjwa”
“Hivi kilicho andikwa hapo unakielewa?”
“Ahaa hata kama”
Nikataka kuchomoa bastola ila nikamuona baba mkubwa akishuka kwenye gari, akatufwata hadi sehemu tulipo. Mlinzi alipo muona baba mkubwa akaanza kutabasamu kwa manaa baba mkubwa ni mtu maarufu sana kwenye mkoa huu wa Tanga.
“Kijana vipi tena”
“Shikamoo mzee”
“Marahaba, fungua geti tuna mgonjwa”
“Ahaa hakuna shida muheshimiwa bwana, sahamani”
“Sawa”
Mlinzi kwa haraka akaelekea getini na kufungua geti, taratibu tumaingiza gari eneo la hospitali, tukazisimamisha sehemu ya maegesho, nikashuka kwenye gari huku nikiwa makini kutazama kila sehemi, nikamfungulia raisi mlango wa nyuma baada ya kuona ulinzi upo salama, akashuka. Walinzi wote wanne tukamuweka kati huku mimi nikiwa ninaogoza sehemu za kuelekea, baba mkubwa na mama wakiwa wanafwata kwa nyuma.
Cha kwanza nikaelekea kwa daktari mkuu wa zamu, tukiwa nje ya mlango wake tukasikia miguno milaini ya msichana ndani humo. Kusema kweli kiroho kikaanza kunidunda kwa maana mchezo huu ndio nilio mfuma nao daktari jana nilipo elekea kutazama Yudia hospitalini kwake.
“Fungu”
Raisi aliniamrisha nikashika kitasa cha mlango, nikausukuma taratibu, ukafunguka. Raisi akaumalizia kuufungua kwa nguvu. Wote tukashuhudia daktari na nesi wakiwa juu ya kitanda maalumu kinacho kuwa katika ofisi ya daktari kwa ajili ya kupumzikia mgojwa. Wakifanya yao tena wakiwa na sare za kazi zao. Nesi akiwa amekipandisha kigauni chake juu, daktari akiwa ameshusha suruali yake chini, na koti lake refu likiwa limemfunika kwa nyuma. Walipo tuona, raisi akatoa simu yake mfukoni na kupiga picha kaza za uchafu wanao ufanya.
Mimacho ikazidi kuwatoka kiasi cha sisi wote kukaa kimya. Wakaanza kupaparika wakijaribu kutaka kuvaa nguo zao.
“Munavaa nini wakati tumesha waona maungo yenu hayo. Hii ndio kazi iliyo waleta hapa?”
Swali la raisi likawafanya daktari na nesi kukaa kimya vichwa wakiwa chini.
“Funga pingu wote hao”
Babyanka sikujua hata ni wapi alipo zitolea pingu hizo, akawafunga kila mmoja pigu yake akaifunga na kitanda hicho cha chuma walichokuwa wanatumia kuburudika.
Tukatoka ofisini humu na kuelekea kwenye wodi za wamama walezi na wajawazito, kila mmoja nikaona akikimbilia kuziba pua yake, kwani harufu kali na mbaya tuliyo kutana nayo mlangoni ilitufanya kufanya tulicho kifanya. Raisi akawa wa kwanza kuingia ndani humu, kila mmoja akaoenekana kushangaa mazingira machafu ya wamama hao wanapo lala. Vitanda vimejaa, huku wengie wakiwa wamelala chini. Hapakuwa na hata sehemu ya kuingilia, wamama wote walipo muona raisi wakaanza kutonyana na kuamshana kumtazama raisi.
“Habari zenu jamani”
“Salama”
Wamama hao wakaitikia kwa pamoja walipo muona raisi, raisi akaka kimya huku akionekana kujawa na simanzi sana kwa hali hii, kwani kuna wamama wana watoto wachanga. Kama sisi watu wazima tumekutana na harufu hii kali na mbaya je hawa watoto wadogo wanao ishi humu ndani nao inakuwaje.
“Nimeona hali munayo pata”
“Kweli baaa, hali ndio kama hii unayo iona. Tunateseka sisi, tunanyanyasika, hata hizo hali za kununulia vitanda hazipo”
Mama mmoja aliye lala kwenye kitanda kilichopo karibu na mlango alizungumza huku akimtazama raisi usoni. Wamama hao kila mmoja akaanza kutoa malalamiko yake, kwa muheshimiwa.
“Nimeona na nimewasikila, nawahakikishia hadi saa moja usiku leo, hali haito kuwa hii humu ndani”
“Tutakushukuru muheshimiwa”
“Watanzania mumenichagua ili niwatumikie. Ni zambi kuona tajiri analalia kitanda cha sita kwa sita wakati huku hospitalini vitanda ni vichache. Hata Mungu hapendi asiii”
“Kwelii”
“Masikini tazama hichi kimalaika cha Mungu kilicho bebwa na huyu mama yangu, kweli ni chakulala chini na mama yake. Ahaa kweli sikubaliani na hili swala”
Raisi alizungumza huku taratibu akichuchumaa, akakibeba kitoto kichanga ambacho imepakatwa na mama yake aliye kaa chini sakafuni.
“Anaitwa nani?”
“Bado sijampa jina, nimejifungua jana jioni”
“Jamani ahaaa, haya mama zangu nimesikia kilio chenu na nyinyi mutaona mabadiliko le oleo”
“Sawa muheshimiwa”
Raisi akamrudisha mtoto huyo kwa mama yake kisha tukatoka katika katika wodi hizi na kuelekea katika wodi nyingine ambapo huko nako tukakuta madudu ya ajabu. Madaktari na manesi hawawajibiki, wanawanyanyapaa wagonjwa hususani wenye hali mbaya sana. Ni daktari mmoja tu kijana ambaye tulimkuta yupo bize akihangaika kuhudumia wagonjwa kwenye moja ya wodi ya wanaume.
“Umeingia zamu yako saa ngapi?”
“Kama siku mbili nyuma hivi muheshimiwa”
“Siku mbili, kuna zamu ya siku mbili mfululizo?”
“Hapana muda wa kufanya kazi ni masaa kumi na mbili kumi na mbili, ila sikuwa na jinsi kwani madaktari wengine wananitegea kila siku wanakuwa na udhulu”
“Ni kweli muheshimiwa, mimi nina wiki nimelazwa kwenye hii hospitali. Ila huyu kijana ana juhudi sana na moyo wa kuipenda kazi yake, ila madakari wengine ni watoro kabisa”
Mzee mmoja aliye lala kitandani alizungumza huku akimtazama raisi usoni.
“Kwenye kitengo chako mupo wangapi?”
“Kumi na tano”
“Kumi na nne wapo wapi?”
“Ndio hao wenye udhulu kila siku”
“Aiseee kumbe ndio utendaji wao wa kazi”
“Ndio muheshimiwa”
“Niandikie majina yao sasa hivi”
Daktari huyo akatoa kijikitabu kidogo cha kumbukumbu kwenye koti lake pamoja na peni, akaanza kurozesha majina ya madaktari wezake, akamaliza na kumkabidhisha raisi.
“Nipelekeni kwenye daftari la maudhurio”
“Sawa mkuu”
Daktari akaongoza nyia, tukafika hadi kwenye chumba ambacho ndipo madkatari wote wanapotakiwa kufika kazini asubuhi wanasaini na pale wanapo toka wana saidi. Raisi akaanza kuligagua daftari hilo, nikaona akitingisha kichwa tu.
“Naombeni koti na mimi leo niwe daktari nikaaa humu kuangali jinsi wanavyo kuja, nyinyi nilindeni kwa nje”
“Sawa mkuu”
Raisi akapewa koti la kidaktari kisha sisi tukatoka nnje ya chumba hichi kuendelea kuimarisha ulinzi. Muda wa kufika ofisini kwa mfanyakazi wa serikali mwisho ni saa moja na nusu tena kwa wale wa mbali ila hadi inafika saa mbili asubuhi hakuna hata mmoja aliye fika, jambo lililo nifanya niwaze sijui ni kitu gani watakacho fanywa na raisi hawa madaktari.
ITAENDELEA

No comments:
Write comments

Recommended Posts × +