Pages

Monday, June 3, 2019

Hizi ni Mbinu za Jinsi ya Kujizuia Kufanya Mapenzi Katika Mahusiano Mapya

Kuingia katika mahusiano mapya ya kimapenzi ama uchumba huwa ni furaha lakini pia inakuweka katika wakati mgumu pia. Unaingiwa na hisia ambazo hujawahi kuwa nazo, Mpenzi wako anakufurahisha na wewe pia unamfurahusha.
Lakini inaweza kuibuka sitofahamu wakati ambapo wewe hutaki ama hujiskii kufanya mapenzi, kwa sababu unataka kuendelea kuwa mwaminifu mpaka siku ile ya ndoa ama sababu yoyote ile nyingine, unayo haki ya kujizuia kutofanya tendo la ngono mpaka ile siku mtakayo funga ndoa na kuwa mwili mmoja. Uwe mwanamke ama mwanamme kumbuka mwili ni wako na maamuzi ni yako.
1. Usilale kwake
Iwapo hautaki kufanya mapenzi na mpenzi wako, basi ni vizuri usijiingize katika hali ambazo zitachangia nyinyi wawili kuingiwa na hamu ya mapenzi . Iwapo umetoka deti na mpenzi wako, usijaribu kumsindikiza hadi kwake ama kuenda njia moja. Pia hutakiwi kuwa unazunguka sehemu ambazo mpenzi wako anaishi wakati kama huo kwa sababu inaweza kuchangia pakubwa kuingiwa na tamaa.
2. Usiwe mlevi
Kuna baadhi ya watu wanafikiria ya kuwa matumizi ya vinywaji ukiwa na mpenzi wako inapunguza hisia za kufanya mapenzi. Well, labda inaweza kuwa ni kweli lakini kulingana na utafiti ni kuwa mtu mlevi anapoteza mwelekeo wa kufanya maamuzi yafaayo. Hivyo ukiwa umeathirika na ulevi pamoja na mpenzi wako, kuna asilimia kubwa ya kufanya maamuzi ambayo si sawa.
3. Toa visababu ambavyo havitomkwanza mpenzi wako
Unaweza kutoa visababu kama vile unaumwa na kichwa, hujiskii vizuri nk. Ingawa kutumia uongo kwa mpenzi wako si jambo zuri, ni muhimu sana iwapo itakuja kwa maswala ya kufanya mapenzi ama kama hujiskii kufanya mambo mengine ambayo yanahusiana na wewe. Hivyo ni muhimu kupatia mambo mengine kipao mbele.
4. Fungua roho yako
Hii ndio njia nzuri zaidi kujizuia kutofanya mapenzi. Kukaa na mpenzi wako katika kikao na kumueleza ndani na nje kuhusiana na wewe kujizuia kutofanya mapenzi ni jambo nzuri zaidi kwa nyote wawili. Kumueleza ukweli mpenzi wako kutatoa ile nafasi ya kwako kuonekana kama unayapenda mahusiano yenu na hauhitaji kuficha ama kudanganya katika mahusiano yenu.
Iwapo atakubali basi itadhahirisha ya kuwa yeye anatilia maanani mahusiano yenu. Kama atakataa basi bila shaka mahusiano yenu hayatokuwa marefu.

No comments:
Write comments

Recommended Posts × +