Pages

Monday, May 20, 2019

AISIIIII……….U KILL ME 26........ ONLY 18+

ILIPOISHIA
Nikaona kijimshale hicho kikipanda juu, ikanibidi kusubiria, Ilipo fika goroda ya nne, mlango ukafunguka. Macho yakanitoka, baada ya kukutana na Yudia akiwa na wanaume wawili wa kisomali huku Yudia akiwa amevalia koti kubwa jeusi. Yudia alipo niona akafungua zipu ya koti hilo, macho yakazidi kunitoka pale nilipo yaona mabomu mawili makubwa, yakiwa yamefungwa kwenye koti hilo huku taratibu yakipungua dakika kueleka katika mlipuko mkali.

ENDELEA
Mapigo ya moyo ukichanganya na kajasho kanako anza kunimwagika, nikabaki nikiwa nimeduwaa. Kwa ishara Yudia akanionyeshea kidole niingie ndani ya lifti hiyo. Sikuwa na ujanja wa aina yoyote kusema labda ninaweza kuchomoa bastola zangu na kufanya shambulizi lolote, kwani kufanya hivi kutapelekea maisha ya watu wengi ndani ya hoteli hii kuweza kupotea kwa mlipuko huu. Nikaingia kwenye lifti hiyo, jamaa mmoja akaanza kunipapasa kuanzia chini hadi juu, akatoa bastola moja baada ya nyingine. Hadi zinafika tano, Yudia yeye mwenyewe akabaki akinishangaa.
“Mvueni na hilo begi”
Hapo ndipo kama nikawa nimegutuka kutoka katika woga na kujitambua kwamba mimi ni nani, nina uwezo gani na nina msaada gani katika taifa langu. Jamaa huyo alipo nisogelea, nikajikuta, nikirusha ngui iliyo mpata kwenye pua, hadi akapiga yowe, nikajizungusha kwa mtindo wa kurusha teke la kulia hewani huku mguu wa kushoto ukiwa umekanyaga chini. Teke hilo likamjumlisha jamaa mwengine wa pili pamoja na Yudia.
Wote wakajibamiza kwenye kuta ya lifti. Sikuishia hapo, kwani nikashusha makonde mengine ya uhakika na yenye ujazo kwa jamaa niliye mpiga ngumi ya pua, akazimia. Yudia, alipo jaribu kuifwata bastola yangu, nikampiga kwenye mguu ambao niliupiga risasi, na kumfanya kulia na kuanguka chini. Sikuwa Dany kama yule aliye nizoea, hapa ninapigana kufa na kupona kwa ajili ya kuyaokoa misha yangu pamoja na kuokoa uaminifu na kazi ya mama yangu.
Nikawahi kuokota bastola yangu, kwa kasi ya ajabu nikampiga riasai mbili za kichwa jamaa niliye mpiga teke. Yudia, akabaki akiwa ameduwaa, akajaribu kulivua koti lenye bomu, nikampiga ngumi ya shingo maeneo ya koromeo na kumfanya ajishike shingo yake huku akiwa ametoa jicho.
“Kroooooo”
Akatoa mlio wa kukoroma, huku taratibu akilala chini. Nikaitazama lifti na kukuta ndio inafika chini. Nikaminya sehemu ya kuizuia mlango usifunguke. Nikalifungua koto la Yudia na kukuta mabomu hayo ya kutegwa yakiwa yamebakisha dakika nne na sekunde kadhaa.
Kwa haraka nikamvua koti hilo, nikachukua bastola zangu zote na kila mmoja nikairudisha sehemu nilipo itoa, nilipo hakikisha kwamba zimekaa sawa, nikampigia Luka simu na kumpa maelekezo ya kuja kumchukua Yudia pamoja na huju jambazi aliye zimia.
“Hapo chini?”
“Ndio sasa hivi njooni nyote”
“Sawa”
Nikaminya kitufe cha kufungua lifti kisha nikatoka kwa kasi ya ajabu sana, kila mmoja akanishangaa. Nikakimbilia sehemu lilipo gari langu, nikalitanguliza koti hilo na kulitupia siti ya pembeni, huku nikivua begi lenye nyaraka za serikali kwa haraka na kulitupia siti ya nyuma, kisha mimi nikaka kwneye siti ya dereva, nikawasha gari, nikaligeuza nyuma kwa kasi hadi waendesha taksi pamoja na bodaboda waliopo kwenye hoteli hiyo wakabaki wakiwa wamenikodolea macho kwa mshanga. Nikaanza kuliendesha gari langu kuelekea maeneo ya Deep Sea. Japo ndani ya gari kuna A/C ila kajasho hakukuacha kutiririka, kwani kila ninavyo tazama dakika za mabomu haya zinazidi kupungua na hadi sasa hivi zimebaki dakika mbili, na sekunde hamsini tu.
Nikazidi kuongeza mwendo kasi wa gari langu kuhakikisha kwamba ninaweza kufika katika eneo nililo kusudia haraka iwezekanavyo, hadi ninafika katika eneo la Deep Sea, sehemu ambayo watu hawaitumii kwa shuhuli za uvuvi, nikashuka kwenye gari na kulitoa koti hilo, huku macho yangu nikitazama mabomu hayo yanavyo zidi kushuka sekunde zake. Yakawa yamebakia dakika moja na sekunde ishirini. Nikaanza kukimbilia baharini kwenye maji, hadi maji yalipo nifika kiwango cha kifua, sekunde za bomu hilo zikwa zimefika sekunde hamsini huku zikieleka kushuka sekunde ya arobaini na tisa.
Kwa nguvu zangu zote nikajirtahidi kulirusha koti hilo la mbali kwenye bahari, kisha kwa haraka nikaanza kurudi kwa kwa kikimbia japo maji ni mazito na yana nguvu, ila ikanibidi kusindana nayo hivyo hivyo. Hadi na karibia kufika ufukweni. Nyuma yangu nikasikia mlipuko mkubwa sana ulio sababisha mimi kurushwa nje, huku maji mengi yakiruka juu.
“Ohoooooo, haha hahahaaaa”
Nilihikuta nikicheka kwa furaha kwani nimeweza kufanikisha zoezi hilo ambalo ni hatari sana kwa maisha yangu. Taratibu nikakaa kitako huku nikitazama maji yanavyo cheza cheza. Mwili wangu mzima nikawa nimelowa kwa maji, nikaitoa simu yangu mfukoni na kukuta ikiwa imezima huku imejaa maji. Nikatoa betri la simu na kulitenganisha na simu. Taratibu nikanyanyuka, kwa mbali nikaanza kuona watu wakikimbilia kuja eneo hili.
“Waswahili bwana”
Nilijisemea huku nikiendelea kujikongoja hadi lilipo gari langu. Watu hao ambao wanaonekana ni wavuvi wakanipita na kueleka walipo sikia mlipuko. Sikutaka kushuhulika nao, nikaingia kwenye gari taratibu nikaliwasha na kuondoka eneo la tukio. Moja kwa moja nikaeleka kwenye hoteli ya Nyinda nilipo waacha wezangu. Nikakuta mkusanyiko mkubwa wa watu, baadhi walipo niona ninashuka kwenye gari wakaanza kunong’onezana. Nikakuta eneo la hoteli zimezungushiwa utepe wa polisi, nikauvuka, askari mmoja akataka kunizuia, nikatoa waleti iliyo lowana na maji, nikaifungua na kumuonyesha kitambulisho changu ambacho kwa bahati nzuri kimetengenezwa kwa plastiki ngumu sana ambayo si rahisi kuharibika.
“Pita mkuu”
Nikaeleka ndani kulipo tokea tukio, nikamkuta Latifa akiwa amesimama mapokezi akizungumza na mmoja wa wahudumu. Nikamfwata na kumshika mkono tukasogea pembeni.
“Vipi watuhumiwa wapo wapi?”
“Luka amekwenda nao polisi”
“Polisi! Kufanya nini?”
“Polisi wamekuja hapa wamewataka basi, tumeona tuwakabidhi kwa maana hii sio kazi iliyo tuleta huku”
“Shitiii naomba simu yako”
Latifa akatoa simu yake, nikamuomba anitafutie namba ya Luka kwenye majina aliyo yaweka kwenye simu yake, akafanya hivyo kama nilivyo mueleza. Nikaiweka simu hiyo sikioni, ikata kwa muda kisha Luka akapokea.
“Ndio Mnyaturu”
“ Ni mimi”
“Vipi Dany?”
“Upo bado na hao watuhumiwa?”
“Hapana, nimesha wakabidhi kwa kamanda msaidizi wa mkoa”
“Ohoooo daaa kwa nini hamkunishirikisha?”
“Hatukujua. Kwani vipi kuna tatizo?”
“Ndio, so umehakikisha wakiingizwa mahabusu?”
“Ndio”
“Hembu nenda kaangalie kama umeondoka hapo eneo la polisi”
“Sawa”
Nikakata simu huku nikiwa nimejichokea kabisa, nikaiingiza namba ya simu ya mama na kumpigia. Mama akapokea simu na kujitambulisha kwamba ni mimi.
“Mbona na namba nyingine?”
“Nakuomba mama uende ukaandae mazingira kwa baba mkubwa”
“Kuna nini?”
“Nakuomba uweze kufanya hivyo na kama upo ofisini, acha kila kitu wewe nenda kwa baba mkubwa”
Kabla mama hajajibu kitu simu hii, ikaingia simu ya Luka, ikanibidi kuikata simu ya mama kwanza na kuisikilizia simu ya Luka.
“Aisee nimekuta wakiondoka tena na gari la kifahari”
“Shiti nilifahamu”
“Daaa sasa hapa kaka inakuwaje?”
“Unaweza kuwafwatilia?”
“Ndio ngoja nijaribu kwa maana mimi nafika hapa ndio nao naona wanaingia kwenye gari aiana ya VX V8 Toyota”
Moja kwa moja nikajua ni upuuzi wa meya, ndio ameufanya.
“Wafwatile na uwe unanipa kila habari inayo endelea kupitia simu ya Latifa”
“Powa kaka”
Nikakata simu na kumrudishia Latifa simu yake.
“Una silaha zako hapo?”
“Ndio, nipo kamili gado”
“Kuanzia sasa tutakuwa tunaongozana”
“Hakuna shida”
Tukatoka nje ya hoteli, nikarudi kwenye gari, kitu cha kwanza kukitazama baada ya kuingia ndani ya gari ni nyaraka ambazo ndio zinatafutwa. Nikazikuta zikiwa salama salimini. Tukaondoka eneo la hoteli na kuelekea Nguvumali kwa baba mkubwa Eddy. Nikapiga honi na geti lake likafunguliwa na mlinzi. Tukashka kwenye gari na moja kwa moja tukaelekea ndani. Nikamkuta mama mkubwa, akiwa amekaa sebleni.
“Karibuni wageni”
“Asante shikamoo mama”
“Marahaba”
Latifa na yeye akasalimia, kisha sote tukaka kweye sofa moja.
“Vipi, jana umeondoka, tukakuhesabu chakula hujatokea?”
“Ahaa mama ni mambo ya hapa na pale tu”
“Mmm haya huyo ndio mkwe wetu?”
“Hapana ni mfanya biashara mwenzangu”
“Ohoooo binti karibu mwaya”
“Asante mama”
“Xaviela na Xaviena wapo wapi?”
“Mmm walitoka asubuhi, sijui hata wamekwenda wapi”
“Baba je?”
“Naye ametoka amekwenda kwenye maswala ya kumpokea raisi kesho si unajua kwamba baba yako ni mbunge”
“Ahaaa, sasa mama naomba uniazime gari lenu moja”
“Lipi hilo?”
“Hiyo Range hapo nje kuna sehemu nahitaji kwenda nalo, si unajua wafanya biashara kama unataka kwenda kuingia mkataba na makampuni makubwa, ukienda na kigari kama hicho cha mama watakuchukulia, ni mbabaishaji fulani hivi”
“Yaani Dany bado hujaacha hizo swaga zako?”
“Ahaa mama niziachie wapi mimi”
“Sawa, ila kuwa nalo makini, kwa maana hilo gari la baba yako halina hata miezi sita, sasa ukilibamiza huo itakuwa tabu nyingine”
“Siwezi kufanya hivyo, alafu mama kama nikipata suti moja kali ya mzee, kidogo maumbo yetu yanaendana”
“Hahahaa wewe mtoto hembu fanya uoee kwa maana kuto kuoa kwako ndio kunakufanya kila siku uwe unanunua mijinzi hiyo”
“Nitaoa mama, ila kwa sasa bado nipo nipo kwanza”
“Wewe sema upo upo kwanza mwisho wa siku uzee huu, sijui utasema bado upo upo au unaenda enda”
Sote tukajikuta tukicheka, mama mkubwa akanyanyuka na kupandisha gorofani. Baada ya dakika tano akashka akiwa ameshika funguoa mkono wa kulia huku mkono wa kushoto akiwa ameweka fuko kubwa la kuifadhia suti.
“Hii suti baba yako analalamika ina mbana bana, so wewe kavae ujaribu”
“Sawa mama”
“Na inashati lake na tai humo ndani”
“Sawa mama, ndio maana nakupendaga sana”
“Ila huko nyuma kwenye makalio kama umelowana umekaa wapi?”
Nikajigusa kwenye makalio nikakuta ni kweli bado nimelowa lowa, japo nguo za juu zimekauka, ila nguo ya ndani ambayo ni boksa bado haijakauka maji. Nikaingia katika chumba cha wagegi, nikaufunga mlango wa ndani, kisha nikatoa bastola zangu na kuziweka juu ya kitanda pamoja na fuko hilo la kiifadhia suti kisha nikavua nguo zangu na kuingia bafuni.
Taratibu nikaanza kuoga huku mawazo mengi yakiwa yanazunguka kichwani mwangu, mtu ambaye ninamfikiria sana ni Yudia, sifahamu ni kitu gani ambacho huyu mtoto amelishwa hadi inafikia hatua anakuiwa mafia tena wa kujitoa muhanga.
“Kuna kitu hapa”
Nilizungumza huku nikeendelekea kuoga. Nilipo hakikisha kwamba nimemaliza nikatoka bafuni. Nikajifuta maji na taulo maalumu nililo likuta ndani ya chumba hichi. Nikafungua zipu ya fuko hili, nikakuta suti nyeusi pamoja na shati jeusi, huku pembeni kukiwa na tai ndefu nyembamba ambayo ni nyeusi. Nikazitoa na kuanza kuvaa suruali ambayo nimeivaa pasipo kutanguliza nguo ya ndani. Suruali ikanikaa vizuri, nikajaribu na shati nalo ambalo likanikaa vizuri kwenye mwili wangu huku likibana misuli mikubwa kiasi ya mikono yangu pamoja na kifua. Nikakunja tai na kuiweka vizuri na kuivaa. Nilipo hakikisha kwamba nimevaa vyote vya umuhimu, nikavaa na koti hilo. Nikajikuta nikitabasamu huku nikiwa nimesimama mbele ya kioo kikubwa cha ‘dreasing table’.
“Daaaa”
Nilijikuta nikizungumza mwenyewe huku nikizunguka zunguka nikijitazama kila kona ya mwili wangu. Nikachukua bastola zangu na kuanza kuzichomeka kwenye kiuno, nikatoka chumbani huku nikiwa nipo peku peku. Sikumkuta Latifa sebleni jambo lililo nipa mashaka kidogo.
“Yupo wapi huyu mama?”
“Yupo nje huko anazungumza na simu”
“Sasa mama hapa bado viatu”
“Aiseee imekukaa hiyo suti?”
“Ndio mama”
“Ngoja nikuletee viatu, watu wanakikuona wanaweza kusema bonge la pedeshee kumbe, mmmm”
“Ndio hivyo mama”
Mama mkubwa akaelekea gorofani, Latifa akaingia ndani huku akionekana ana wasiwasi mwingi na simu yake akiwa ameishika sikioni. Alipo ona mama mkubwa hayupo, akaniwekea simu sikioni huku akihema akishindwa kuzungumza kitu chochote.
“Halooo”
“Halooo Dany, nimekuja wewe ni nani sasa. Na hapa ninapo zungumza nina mtu wako anaitwa Lukasi msikilizee anacho kipata”
“Ahaaa, nakufaaaaa, uuuuuuuuuu”
Nilisikia sauti ya Luka akilia kwa uchungu mkali akionekana kukupoea kipigo kikali sana kutoka kwa watu walio mkamata na sauti hii sio ngeni kabisa kwangu kwa maana ni meya niliye toka kumkoromea masaa machache nyuma.
“Rafiki yako anaelekea kufa sasa, usipo leta Nyaraka ndani ya nusu saa, baba kijacho anakwenda kuiaga dunia Paaaaaaaaaaaaaaaaaaa”
Nikasikia mlio wa risasi, kisha simu ikakatwa, na kujikuta nikitazamana na Latifa anaye mwagikwa jasho uso mzima.
ITAENDELEA
ITAENDELEA

No comments:
Write comments

Recommended Posts × +